Wazazi wa mtoto wa miezi 15 Dominic
Lacey Wilson kutoka jimbo la Michigan nchini Marekani aliyehudumiwa
pombe kwa bahati mbaya katika mgahawa wa Applebee wiki iliyopita,
wamefungua jalada la kesi dhidi ya kampuni miliki ya mgahawa huo
kutokana na tukio hilo wakidai fidia.
Wazazi hao Taylor Dill-Reese na
Dominic Wilson wamefungua kesi hiyo katika mahakama ya Oakland ambako
ndiko ulipo mgahawa huo, wakilalamika kuwa walipatwa na msongo kufuatia
tukio hilo na kudai kupata hasara ya fedha kwa ajili ya matibabu ya
motto huyo.
Ijumaa iliyopita familia hiyo
ilitembelea katika mgahawa wa Applebees uliopo Madison Heights ambapo
pamoja na mambo mengine waliagiza chakula cha mtoto kwa ajili ya Dominic
ambacho kingekwenda sambamba na juisi ya epo.
Badala yake kinyaji alicholetea
mtoto huyo ni margarita yenye kilevi ambapo baada ya kunywa mtoto huyo
alianza kufanya vitendo vya ajabu vilivyopelekea wazazi wake kushangaa
kwa kuwa sio kawaida yake.
Alipopelekwa katika hospitali ya
karibu damu yake iligundulika kuwa na kilevi kiwango cha 0.10, ambacho
ni kikubwa kuliko kiwango kilichowekwa na mamlaka ya Michigan kwa
madereva cha 0.08. Mtoto huyo pia alipatwa na maumivu ya kichwa, mafua
na mning’inio (hangover) kwa siku kadhaa baada ya tukio hilo.
Mwanasheria wa familia hiyo
William Stern amesema hii sio mara ya kwanza kwa mgahawa huo kuchanganya
vinywaji na pombe kwa watoto.
|
0 comments:
Post a Comment