TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, March 3, 2011

Waziri Huvisa azungumzia maadhimisho ya mazingira afrika leo

6:11 PM



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Terezya Huvisa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Mazingira ya Afrika. kulia ni Ofisa mkuu wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Esther Makwaia na Msaidizi wa Waziri, Bw. Joseph Qamara leo kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli Mjini Dar es salaam.(Picha na Ali Meja)

Nguvu Kazi Gongo la Mboto na UhuruOne


Mdau Mihayo (kulia) na mafundi wakitandika bati

Ndugu yetu Ankal!

Wikiendi hii tulikwenda kuungana na ndugu zetu wa Gongo la Mboto kuona wapi tungeweza kushirikiana kupunguza makali ya maafa yaliowakumba. Tulipopata taarifa kwamba kuna shule 8 zimeathirika tukaona ni bora tuelekeze nguvu zetu huko ili wadogo zetu na walimu wao warudi kwenye hali ya kawaida haraka iwezekanavyo.

Basi tulikwenda kwenye shule ya sekondari ya Juhudi na kutathmini maafa yaliyowapata na Jumapili tulirudi tena na vifaa vya ujenzi na kuanza kuchapa kazi. Jumatatu tuliendelea na kazi na panapo maajaliwa leo tutakuwa tumemaliza kukarabati kuta zote, nguzo na kubadilisha mabati yote 12 yalioathirika.

Tunatanguliza shukurani kwa Mkuu wa Wilaya Mh. Leonidas Gama kwa kujiunga nasi kwenye nguvu kazi hii. Shukurani pia kwa Afisa Elimu wilaya na ofisi ya Mhandisi ya Wilaya kwa ushirikiano wao wa karibu na kwa mwenyeji wetu Mwl Mkuu tunamshukuru sana. Panapo maajaliwa tutarudi kumalizia kupaka rangi baada ya wiki.

Wako katika ujenzi wa Taifa
UhuruOne team.
--
Mdau Rajabu Katunda akipiga kazi
Sehemu mojawapo inayohitaji ukarabati shuleni hapo
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Leonidas Gama akipiga chepeo.
Chini ukarabati unaendelea

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA