Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini TFF, Mwenyekiti wa Shirikisho la
Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) na Mjumbe wa
CAF Bw Leodger Tenga akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za
shirikisho hilo leo wakati alipotoa shukrani zake za dhati kwa Watanzani
na Wana Afrika Mashariki waliomuunga mkono wakati alipokuwa akiwania
ujumbe wa CAF huko Sudan hivi karibuni ambapo alichaguliwa kuwa mjumbe
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika CAF.
Tenga amesema anajua kazi ni kubwa
kwakuwa sasa ana majukumu hapa nchini kama Rais wa TFF, ana majukumu
mengine kwa ajili ya Shirikisho la Vyama Vya michezo wa Miguu Afrika
Mshariki kama Mwenyekiti wa CECAFA na jukumu la mwisho ni la ujumbe wa
CAF akaongeza kwamba "Nashukuru kazi yangu kubwa kama mjumbe wa CUF
itakuwa ni kuwakilisha TFF na SECAFA hivyo ninao uzwezo wa kumudu
majukumu hayo hasa ukizingatia kwamba mimi ni muumini wa Vipindi vya
uongozi na katika majukumu haya vipindi vyangu viwili vitanitosha
nitawapisha wengene waendeleze mambo ambayo nimekwishayaanza" katika
picha kulia ni Msemaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF
Boniface Wambura.
WAZIRI MKUU ATAKA TAARIFA ZA CAG KUHUSU MATUMIZI YA HALMASHAURI.
WAZIRI
MKUU Mizengo Pinda amesema anataka apatiwe taarifa za Mkaguzi Mkuu na
Mdhibiti wa Fedha za Serikali kuhusu matumizi na mapato ya kila
Halmashauri ili apate picha kamili ya matumizi ya fedha za Serikali.
Ametoa
kauli hiyo leo mchana (Ijumaa, Machi 4, 2011), mara baada kuwasili
mjini Bukoba na kusomewa taarifa ya mkoa wa Kagera na Mkuu wa Mkoa huo,
Bw. Mohammed Babu. Waziri Mkuu yuko mkoani hapa kwa ziara ya siku nane
ambako atakagua shughuli mbalimbali za maendeleo kwa kutembelea wilaya
zote za mkoa huu.
Akizungumza
na viongozi mbalimbali wa mkoa huo, Waziri Mkuu alisema kuna haja ya
kumpatia taarifa hiyo juu ya ukaguzi uliofanywa na ofisi ya CAG. “Uzuri
wa taarifa wa hiyo unaonyesha nani kapata nini na katumia vipi, pia
utaona ni Halmashauri zipi zimepewa ripoti safi na zipi zimepewa ripoti
chafu,” alisema.
Alisema
Serikali inatuma fedha nyingi mikoani na katika Halmashauri kupitia
miradi mbalimbali lakini matokeo halisi ya fedha hizo hayaonekani katika
maisha ya Mtanzania wa kawaida.
Akitoa mfano, alisema fedha nyingi inatolewa katika Miradi ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (DADPS) lakini impact
yake kwa jamii haionekani. “Mkuu wa Mkoa inabidi ufuatilie kwa karibu
matumizi ya fedha hizi kwa sababu kuna watu wametulia tu wanafanya
watakavyo wakijua RC hawezi kufuatilia hadi miradi ya wilayani,”
alionya.
“Mkoa
wa Kagera umepata sh. bilioni 10 kwa ajili ya miradi ya DADPS na ninyi
mna wilaya saba, maana yake ni kwamba kila wilaya ina zaidi ya
sh.bilioni moja na ushee lakini kama fedha hii haionekani imefanya nini,
hali inatisha!”
Akizungumzia
kuhusu kero za wananchi, alishauri Mkuu wa Mkoa na kila Mkuu wa Wilaya
watenge siku maalum za kusikiliza wananchi na kuwapatia suluhisho kwa
matatizo hayo na kwa yale yaliyoshindikana, wapeleke taarifa ngazi za
juu.
Kuhusu
elimu, alisema mkoa unakabiliwa na tatizo la mimba hali ambayo alisema
hairidhishi kutokana na idadi kubwa ya wasichana waliopata ujauzito.
“Katika mwaka 2009/2010 jumla ya watoto 339 waliacha shule kutokana na
ujauzito na kati yao 70 ni wa shule ya msingi… hii inatisha. Ongeeni na
wazazi na walimu, lakini zaidi watafuteni wakosaji, wakiwekwa ndani hata
watu 10, basi watajua kuwa hili ni baya,” alisisitiza.
Akizungumzia
matatizo ya mkoa kwa ujumla, Waziri Mkuu alisema ataendelea kufuatilia
tatizo la takwimu kwani anataka kubaini ni kwa nini mkoa wa Kagera kwa
miaka mitano mfululizo umekuwa miongoni mwa mikoa mitano ya mwisho
kwenye Kiashiria cha Kipato cha Wastani wa Mwananchi (Per-Capita Income)
wakati una rasilmali za kutosha na fursa nyingi za uzalishaji.
Aliitaja
mikoa mitano ya mwisho ambayo iko chini ya wastani wa Kitaifa wa pato
la mtu ambalo limefikia sh. 693,470 kwa mwaka; ni Kigoma ulioko nafasi
ya 17 ukiwa na wastani wa pato la mwananchi la sh. 483,158; Shinyanga wa
18 (sh. 455,000); Kagera wa 19 (sh. 453,235); Dodoma wa 20 (sh.
414,597) na Singida ambao ni wa mwisho ukiwa na wastani wa sh. 373,694.
Mchana
huu, Waziri Mkuu anatarajiwa kuzindua barabara ya Zamzam na kuzungumza
na wakazi wa Manispaa ya Bukoba katika uwanja wa Mayunga (Uhuru
Platform).
Kesho
(Jumamosi, Machi 5, 2011), Waziri Mkuu atakwenda wilaya ya Muleba
ambako atakagua shamba la mkulima bora wa kahawa katika kijiji cha
Ilogero kabla ya kwenda Buganguzi ambako atakagua mashamba ya migomba
ambayo yameshambuliwa na magonjwa ambayo mpaka sasa hayajajulikana
kisayansi. Pia ataweka jiwe la msingi katika mradi wa umwagiliaji wa
kijiji cha Buyaga na kuhutubia wananchi katika viwanja vya Shule ya
Msingi ya Kasharunga.
Kesho
kutwa (Jumapili, Machi 6, 2011), Waziri Mkuu atakuwa wilayani Chato
ambako anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika jengo la Halmashauri ya
Wilaya hiyo na kufungua SACCOS ya Mshikamano kabla ya kuzungumza na
wananchi katika mkutano wa hadhara kwenye shule ya msingi ya Chato.
WAZIRI EZEKIEL MAIGE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA UTALII DOUBLE TREE.
Waziri
wa Maliasili na Utalii Mh. Ezekiel Maige akifungua mkutano
uliokutanisha wadau wa Utalii nchini ambao umeanza leo kwenye hoteli ya
Double Tree Hilton jijini Dar es salaam, mkutano huo utajadili mambo
mbalimbali na changamoto zinazokabili sekta ya utalii nchini na kuweka
mkikakati ya kukwamua sekta hiyo ili kuutangaza vyema utalii wa Tanzania
ndani na nje ya nchi hivyo kuongeza idadi ya watalii.
Mkurugenzi
wa Bodi ya Utalii nchini TTB Bw Aloyce Nzuki akimkaribisha Mh. Ezekiel
Maige Waziri wa Maliasili na Utalii kwa ajili ya kufungua rasmi mkutano
wa wadau wa utalii ulioanza leo jijini Dar es salaam.
Peter
Mwenguo katikati ambaye ni Mkurugenzi Mstaafu wa Bodi ya Utalii (TTB)
ni moja wa washiriki wa mkutano huo Peter Mwenguo ni hazina ya uzoefu
kwani amekuwepo katika sekta ya utalii na kufanya mkazi kwa muda mrefu
kulia ni Madanga Shaban Madanga pamoja na mshiriki mwingine wa semina
hiyo.



0 comments:
Post a Comment