Rais Barrack Obama wa Marekani amekashifu machafuko
yanayo endelea nchini Libya, katika hotuba yake ya kwanza kwenye runinga
tangu mageuzi yaanze nchini Libya, yapata wiki moja sasa.
Amesema kuwa ukatili unaotumiwa na vyombo vya serikali kukabili waandamanaji haukubaliki kamwe na kuwa serikali yake inatathhmini hatua za kuchukua.
Amesema kuwa ukatili unaotumiwa na vyombo vya serikali kukabili waandamanaji haukubaliki kamwe na kuwa serikali yake inatathhmini hatua za kuchukua.
Japo hakutoa maelezo zaidi, alidokeza kuwa
waziri wa mashauriano ya nje Hillary Clinton atasafiri mjini Geneva,
Uswizi, kushauriana na nchi zingine.
Huku hayo yakiarifiwa maelfu ya waandamanaji wanaopinga serikali
wamekuwa wakisherehekea kile wanachokiita ushindi mkubwa Mashariki mwa
Libya.
Wakaazi mjini Tripoli wamesema wanaogopa kutoka
nje kwa sababu wana wasiwasi wanajeshi wanaounga mkono serikali huenda
wakawafyatulia risasi.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema
yamethibitisha kuwa watu wasiopungua mia tatu wameuwawa tangu
makabiliano hayo kuanza wiki iliyopita.

0 comments:
Post a Comment