TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Friday, December 10, 2010

SHEREHE ZA UHURU WA TANZANIA BARA KATIKA PICHA

8:41 AM


Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mohammed Gharib Bilali, akisalimiana na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, katika sherehe za miaka 49 ya Uhuru ziliofanyika jana uwanja wa uhuru Jijini Dar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohammed Shein,akisalimiana na Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe.Benjamin Willium Mkapa, katika sherehe za miaka 49 ya Uhuru ziliofanyika jana uwanja wa uhuru Jijini Dar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk Shein akisalimiana na Mkuu wa majeshi Tanzania.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Mrisho Kikwete, akiwasalimia wananchi waliohudhuria sherehe za Miaka 49 ya Uhuru , zilizofanyika jana Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.



Vikosi mbali mbali vya Ulinzi na Usalama vya Jeshi,Polisi,JKT,Mafunzo na Wanamaji wakipita mbele ya Rais wa Jakaya Mrisho Kikwete na kutoa salamu ya Heshima kwa Gwaride katika kushereheka miaka 49 ya Uhuru.






Vijana wa Halaiki wakicheza halaiki kwa maamkizi kwa wageni waliohudhuria katika sherehe za miaka 46 ya Uhuru,zilizofanyika jana,Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Jakaya Mrisho Kikwete,akikagua Gwaride rasmi la majeshi ya Ulinzi,wakati wa sherehe za miaka 49 ya Uhuru wa Tanganyika.

Ndege za Jeshi la wananchi zikipita angani kusalimia,katika sherehe za Uhuru kutimia miaka 49 uwanja wa Uhuru Jijini Dar.





Wananchi waliohudhuria sherehe za Uhuru. Picha na Ramadhan Othman, Ikulu
Askari wa Kikosi cha Jeshi la Polisi cha Kutuliza Ghasia (FFU), akilinda usalama wakati wa maadhimisho hayo. Askari huyo ni miongoni mwa askari waliokuwa wanalinda msafara wa rais.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA