Rais wa Kampuni ya RBP Oil & Industrial Technology Tanzania LTD,Mama Rahma Al. Kharoos akizungumza leo wakati akitangaza kuisaidia Taasisi ya Popular Sports and Entertainment ambayo imeandaa Bonanza la watoto wapatao 600 toka katika vituo 10 vya kulelea watoto yatima vya jijini Dar.Mama Rahma Al-Kharoos ametoa kiasi cha sh. Milioni 4 taslimu kwa ajili ya kuwezesha kufanyika kwa tamasha hilo siku ya jumapili,Novemba 21 katika viwanja vya Lidaz Klabu.
Rais wa Kampuni ya RBP Oil & Industrial Technology Tanzania LTD,Mama Rahma Al. Kharoos akimkabidhi kitita cha sh. milioni 4, Mkurugenzi wa Taasisi ya Popular Sports and Entertainment Tanzania ambao ndio waratibu wa Bonanza hilo,Osman Kazi katika hafla fupi ya makabidhiano hayo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Coco Beach,jijini Dar.
0 comments:
Post a Comment