TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, November 17, 2010

Mwana Mfalme William kuoa

2:08 PM


Mwana mfalme William atafunga ndoa na Kate Middleton mwaka ujao, kwa mujibu wa taarifa kutoka jumba la kifalme jijini London, Clarence House.

William

Kate Middleton na Mwana Mfalme William

William, ambaye ni mrithi wa pili wa kiti cha ufalme, atafunga ndoa mwakani, katika mwaka ambao ungeadhimisha miaka 30 ya ndoa ya wazazi wake.

Wawili hao waliweka ahadi ya uchumba mwezi Oktoba nchini Kenya, wakati wakiwa katika mapumziko.

Kate

William na Kate kufunga ndoa

William na Kate walianza kuwa na mahusiano miaka minane iliyopita, wakati wakisoma katika chuo kikuu cha cha Mtakatifu Andrews huko Fife, ambapo pia waliishi katika nyumba moja.

Ndoa hiyo imetangazwa katika taarifa fupi iliyotolewa na Clarence House.

Taarifa

Taarifa hiyo imesema: "Mwana Mfalme wa Wales, ana furaha ya kutangaza ndoa ya mwanae, Mwana Mfalme William atakayofunga na Bi Catherine Middleton.

"Harusi itafanyika wakati wa majira ya joto ya mwaka 2011, mjini London. Taarifa zaidi kuhusu harusi hiyo zitatangazwa baadaye.

"Mwana Mfalme William amemfahamisha Malkia na ndugu wengine wa karibu.

Kate

Kate na William

"Mwana Mfalme William pia ameomba ruhusa kutoka kwa baba wa Bi Kate.

"Baada ya kufunga ndoa, wawili hao wataishi kaskazini mwa Wales, ambapo Mwana Mfalme William ataendelea na kazi katika jeshi la Anga la Uingereza Royal Air Force."

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA