TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, March 31, 2010

Albamu ya Wagosi hatimaye yaingia sokoni

4:28 PM

Baada ya kukwaruzana na Serikali na kulazimishwa kusimamishwa kuingia sokoni kwa Albamu ya Wagosi wa Kaya inayojulikana kama
“miaka 10 ya maumivu” hatimaye albamu hiyo imeruhusiwa na serikali.

Akiongea na mtandao huu kitaa mmoja wa wanamuziki wa kundi hilo Mkoloni amesema kuwa “tuliambiwa tubadilishe baadhi ya maneno kwenye baadhi ya nyimbo ambayo kimsingi serikali iliona kuwa na uchochezi na tumefanya hivyo” alisema Mkoloni. Sasa mambo ni shwari na Mpango mzima uko sokoni.

Vijana wa Muziki wa kizazi kipya wamekuwa wakiimba mara nyingi kuhusu mapenzi ni mara chache kwa vikundi au mtu mmoja mmoja anaamua kushikia bango matatizo ya kijamii jambo ambalo lingekuwa jukwaa zuri la kufikisha ujumbe wa machungu ya wananchi huku chini. Kila la heri wagosi.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA