Vyombo vya habari vimeangazia ripoti ya Umoja wa Mataifa ilioashiria kuwepo kwa wapiganaji wa Al Shabaab nchini Kenya. Ripoti hiyo pia inadai kuwa nusu ya wapiganaji wa kundi hilo ni raia wa Kenya.
Lakini katibu katika wizara ya usalama wa ndani Francis Kimemia, ameiambia BBC kuwa madai hayo ya Umoja wa Mataifa, hayana msingi wowote na kuwa hakuna mzazi yeyote mkenya anaweza kuwaruhusu watoto wake kwenda kuuawa nchini Somalia.
Kimemia pia amekanusha madai kuwa viongozi wa Al Shabaab wanaishi mjini Nairobi. Wapiganaji wa Al Shabaab wametishia mara kadhaa kuishambulia Kenya, kwa kuwa inasaidia serikali ya mpito ya nchi hiyo na hapo jana wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wa kundi hilo walishambulia wanajeshi wakiwa kwenye doria Kaskazini mwa Kenya.
0 comments:
Post a Comment