TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, April 1, 2010

BIRTHDAY YA NICE CHANDE KATIKATI YA BAHARI ILIVYOFANA

1:16 AM


Wadau wangu baada ya kuwaambia kuwa nitawaletea part 2 ya picha za Birthday ya Nice Chande iliyofanyika ndani ya Boat na kuwa gumzo ndani ya Jiji la Dar es salaam leo nimeamua kuwaleteeni matukio mengine yaliyojiri ndani ya Boat na kisiwani Bongoyo,Sherehe hii ilikusanya baadhi ya mastaa wa bongo ilifanyika na kumalizika kwa amani bila mtu yeyote kudhuriwa na hakuna vitendo vyovyote vile vibaya vilivyotokea, hongera muandaaji na waalikwa

Swahiba alijiandaa kabisa kabla ya hatari hapa akiwa na Silvanus Mwilu

Wadau wa Birthday wakijipongeza

Huyu jamaa anaitwa Mussa wa kipindi cha Uswazi Eatv yeye ndiye alikuwa Mc wa shughuli nzima kwakweli jamaa ni bonge la Mc aliendesha shughuli kwa umakini mkubwa sana Big up kaka nikiwa na shughuli yangu lazima nikuite

Auntie Ezeckiel akiwa anaangalia ampake nani cake usoni

Muziki ulifunguliwa rasmi na Mc, hapa mambo ya Mtalimbo umelala doro

Birthday gal akifungua muziki kwa kucheza Yori yori

Ilikuwa zamu ya Yusuph Mlela kucheza Yori Yori,hapa ilikuwa kila mmoja lazima acheze huu wimbo

Ilifika zamu ya Mc Mussa kukata mauno jamaa anayaweza kama kichura wa Eatv

Mambo ya Jackline Wolper hayo

Sauda Mwilima huyo na mambo ya Yori yori

Jamani kisigino kilikuwa live siku hiyo
Uliwadia muda wa usiku na burudani zikaendelea kama kawaida,Hapa ni kisiwani Bongoyo

Ndani ya Boat zilipigwa sebene za kufa mtu

Birthday gal Nice Chande akicheza mpira ndani ya kisiwa cha Bongoyo

Shangwe zikiendelea kama kawa

Hongera Nice Chande watu walifurahi sana

Tinno akicheza ngoma za Kwaito

Mambo yameshashika kasi tayari,Mlela akiwa juu kabisa ya Boat

Camera man Farid Uwezo mambo yalimzidi ilibidi aweke camera pembeni

Mc akimwangalia Tino akifungua champagne
Champagne ilifunguliwa kuashiria upendo kwa Nice Chande na waalikwa wote

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA