TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Monday, September 28, 2009

Polanski atiwa mbaroni baada ya miaka 30

7:57 PM

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Bernard Kouchner, amesema yeye na mwenzake wa Poland wamemuandikia waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, kuhusu kukamatwa kwa muongozaji wa filamu , Roman Polanski.

Akizungumza katika radio ya Ufaransa Bwana Kouchner amekielezea kitendo cha kukatwa kwa Polanski kama ni ukatili. Bwana Polanski ambaye ana uraia wa Ufaransa na Poland alitiwa nguvuni siku ya jumamosi nchini Switzerland.

Vyombo vya sheria mjini Los Angeles wanataka bwana Polanski arejeshwe Marekani ili ahukumiwe kwa kufanya ngono na binti wa miaka 13 hapo mwaka 1977.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA