TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Friday, August 14, 2009

Taiwani yaongeza juhudi za uokoaji

3:15 PM
Serikali ya Taiwani imetuma askari zaidi ya 4000 kuongeza juhudi za uokoaji huko maeneo ya kusini kuliko athiriwa na kimbunga, ambapo maji yanyoendelea kujiskusanya yakisababisha tishio jipya kwa vijiji ambavyo vilinusurika na kimbunga cha kwanza cha

Morakot. Serikali imethibistisha, vifo zaidi ya 100 vimetokana na Morakot ambacho kimetiririsha mvua zaidi ya mita 2 kisiwani humo mwishoni mwa wiki iliyopita, kikiwakumbusha watu mafuriko makubwa yaliyowahi tokea miaka 50 iliyopita.

Mpaka sasa watu wapatao 108 wameshauawa na mafuriko hayo, lakini idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka.

Helikopta zilikuwa zikitafuta maeneo ya kusini mwa Taiwan na kuwaangushia vyakula kwenye vijiji ambavyo vimejitenga kutoka na barabara za kufikia huko kuharibiwa na mmomonyoko wa ardhi.

Watu karibia 14,000 wamehamisha kwa njia ya helokopta kupelekwa kenye usalama tangu mwishoni mwa wiki

Lakini walionusurika na wanasiasa wanaishutumu serikali kwa kuchelewa kidogo kwa shughuli hizo za uokoaji. Mwanakijiji mmoja alisema "hatukusaidiwa, tulisahaulika, tulikuwa tunasubiri helikopta bila kitu chochote"



0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA