TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, July 28, 2012

Rais Jakaya Kikwete Azindua Karakana na Ndege za Shirika la Ndege La Precision Air

3:15 PM
 Rais Jakaya Kikwete akiweka mkasi mara baada ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Karakana na ndege za shirika la ndege la Precision Air jana kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jijini Dar es salaam kulia ni Bw Bw. Michael Shirima
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya shirika la ndege la Precision Air Bw. Michael Shirima katikati mara baada ya kuzindua Karakana ya ndege za shirika hilo, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Precision Air Bw. Alfonce Kioko
Rais Jakaya Kikwete akihutubia wageni waalikwa katika uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la ndege la Precision Air Bw. Michael Shirima akimkabidhi zawadi Mh Rais Dk. Jakaya Kikwete mara baada ya kuzinduz rasmi karakana na ndege za shirika hili (Hanga) kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jana jijini Dar es salaam, Karakana hiyo itakuwa na ikihudumia ndege za shirika hilo la mashirika mengine pia lakini pia itapokea wanafunzi walio kwenye mafunzo ya Uinjini wa ndege kutoka katika vuo vya ndani.
 Mmoja wa mainjinia wa ndege za shirika hilo akirekebisha moja ya ndege za shirika hilo iliyoko kwenye (Hanga) Karakana hiyo.
Rais Jakaya Kikwete akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Precision Air Bw. Alfonce Kioko alipokuwa akitoa maelezo  wakati wakati Rais alipokuwa akikagua  Hanga hiyo, kulia ni Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe 
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Hoteli ya Kibo Palace ya jijini Arusha
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mzee Peter Kisumo mara baada ya uzinduzi huo kulia ni Mkurugenzi wa Hoteli ya Kibo Palace ya Arusha.
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.
 Wafayakazi wa Precision Air wakiwa katika hafla hiyo ya uzinduzi.
 Mkurugenzi wa Hoteli ya Kibo Palace ya Arusha Bw Vicent Laswai naye amehudhuria katika uzinduzi huo kama mdau wa Utalii.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe pamoja na wakuu mbalimbali wa shirika la ndege la Precision Air na wafanyakazi wa shirika hilo mara baada  ya uzinduzi wa (Hanga) hiyo

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA