
Palikuwa hapatoshi jioni ya leo ndani ya ukumbi wa maraha wa Sun Cirro,Sinza jijini Dar.

Kundi la Chocolate lionesha mbwembwe zake jukwaani kuwani kitita cha shilingi milioni moja.

Kundi
la Mazabe Ndonga likionesha umahiri wa kucheza jukwaani kwenye shindano
la kumsaka mshindi wa Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha
maraha cha Suncirro,Sinza jijini dar.Katika shindano hilo yamejitokeza
makundi saba ambayo yameshindana vikali katika kumsaka kinara wao,zawadi
katika shindano hilo ambalo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya bia ya
Serengi,ni fedha taslimu shilingi Milioni moja.Mashindano haya
yamekwishafanyika katika mkoa wa Arusha ambapo mshindi lilikuwa kundi la
Contegious Crew,Zanzibar likashinda kundi la B-Six na mkoani Tanga
kundi la Questions Crew waliibuka washindi,aidha makundi yote hayo
yalijinyakulia kitita cha shilingi milioni moja.

Kundi la Manzese Crew likisaka ushindi kwa udi na uvumba jukwaani kuwania kitita sh milioni moja.

Mmoja
wa wasanii wa kundi la The Ridder akionesha mbwembwe zake kwa mashabiki
kibao (hawapo pichani) waliofika kwenye shindano hili jioni ya jana,ambalo lilikuwa na msisimko mkubwa .

Mc
wa shindano zima,Nickson akiwayataja makundi yaliyotinga fainali kwenye
mchakato wa kulipata kundi kinara la Serengeti dance la Fiesta 2012.

Mmoja wa majaji katika mashindano hayo Isakwisa Thomson akielezea jambo wakati shindano likiendelea.

Mmoja
wa majaji wa shindano hilo Isakwisha Thomson kutoka Clouds FM
akifafanua jambo,kati ni Msami kutoka THT pamoja na B-Dozen kutoka
Clouds FM,Wote ndio waratibu wa shindano hilo la Serengeti dance la
Fiesta 2012.

Kundi
la The Chocolate Crew likishangilia kitita cha shilingi milioni moja
mara baada ya kuibuka washindi kati ya makundi saba yaliyojitokeza
kushiriki shindano la Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha
maraha cha Suncirro,Sinza jijini Dar.Katika shindano hilo kulikuwepo na
ushindani mkubwa lakini mwisho wa siku mshindi ilikuwa ni lazima
ajulikane/apatikane.Shindano hilo ambalo mdhamini wake mkuu ni kampuni
ya bia ya Serengiti ndio mdhamini mkuu wa tamasha kubwa lijalo la Fiesta
linalorajiwa kuanza hapo baadae mara baada ya mwezi mtukufu wa
Ramadhani kuisha.Shindano la namna hii limekwishafanyika katika mkoa wa
Arusha ambapo mshindi lilikuwa kundi la Contegious Crew,mkoani Tanga
kundi la Questions Crew waliibuka washindi pamoja na Viswani Zanzibar
ambapo kundi la B-Six lilishinda.Aidha makundi yote hayo yalijinyakulia
kitita cha shilingi milioni moja.

Baadhi ya mwashabiki wakishangilia

Baadhi
ya washabiki waliojitokeza jioni ya jana kwenye shindano la kumsaka
mshindi wa Serengeti dance la Fiesta 2012,ndani ya kiota cha maraha cha
Suncirro,Sinza jijini dar

Mashabiki wakifuatilia shindani hilo jioni ya jana

Majaji wakijadiliana jambo kumpata mshindi

Mmoja
wa watangazaji wa Clouds TV,Babu wa Kitaa kupitia kipindi Bibi Bomba
akiwa amepozi na wadau wengine wa Clouds Media Group wakifuatilia
shindano la Serengeti dance la Fiesta 2012.
0 comments:
Post a Comment