Mwananchuo
wa chuo cha ualimu cha ST Aggrey kilichopo uyole jijini mbeya anasadikiwa
kufariki dunia baada ya kupigwa na wananchi wenye hasira kali katika maeneo ya
Isanga kwa tuhuma zakuiba pikipiki zakusafirishia abiria maarufu kama bodaboda.
Mmoja
wa mashuhuda wa tukio hilo PRAY GOD MGONJA amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni
VEDASTO PIUS anayekadiriwa kuwa na umri kati 25 mpaka 30 .
Mgonja
amesema tukio hilo limetokea mnamo july 2 mwaka huu majira ya saa 8 za mchana
katika daraja lilopo karibu na hotel ya Rift Valley barabara yakuelekea isanga
jijini mbeya.
Amesema
mtuhumiwa amekumbwa na mkasa huo baada yakupewa taarifa za kuibiwa kwa pikipiki
yenye No T 438BZU aina T-BETTER yenye alama ya chama cha Demokrasia na maendeleo
mali ya JOSEPH KAPASI(23)mkazi wa Ilomba jijini hapa
Kwaupande
wake mmiliki wa pikipiki hiyo JOSEPH KAPASI amesema aliombwa kumfundisha
mtuhumiwa huyo na baadae alipoanza kuendesha vizuri alitokomea nayo na marabaada
ya hapo alipatikana eneo la isanga akielekea barabara ya chunya ili aibe na
ndipo akakamatwa na wanainchi wenye hasira kali nakuanza kumpa kichapo ambacho
kimemfanya azirai.
|
0 comments:
Post a Comment