TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, June 21, 2012

VODACOM TANZANIA MDHAMINI MKUU WA MAWASILIANO NA MATANGAZO SABASABA(TAN TRADE)2012

7:47 PM
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania(Tan Trade)Bw.Samwel Mvingira(kulia)akimsikiliza  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Joseline Kamuhanda,wakati alipokuwal akimwelezea ubora na matumizi ya modem ya Vodacom kwa ajili ya Mawasiliano wakati wa Maonyesho  ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)yatakayoanza  hivi karibu jijini Dares salaam,Vodacom Tanzania ndiyo wadhamini wakuu wa Mawasiliano  na matangazo kwa vyombo vya habari katika kipindi chote cha Maonyesho hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania(Tan Trade)Bw.Samwel Mvingira(kulia)akipokea  modem  pamoja na simu ya mkononi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Joseline Kamuhanda,kwa ajili ya Mawasiliano wakati wa Maonyesho  ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)yatakayoanza  hivi karibu jijini Dares salaam,Vodacom Tanzania ndiyo wadhamini wakuu wa Mawasiliano na matangazo kwa vyombo vya habari katika kipindi chote cha Maonyesho hayo.
  Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania(Tan Trade)Bw.Samwel Mvingira(kulia)akipokea  simu ya mkononi kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Joseline Kamuhanda,kwa ajili ya Mawasiliano wakati wa Maonyesho  ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)yatakayoanza  hivi karibu jijini Dares salaam,Vodacom Tanzania ndiyo wadhamini wakuu wa Mawasiliano na matangazo kwa vyombo vya habari katika kipindi chote cha Maonyesho hayo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bi.Joseline Kamuhanda,kiongea na waandishi wa habari wakati wa kutangaza kampuni ya Vodacom Tanzania kuwa mdhamini mkuu wa Mawasiliano na matangazo  wakati wa Maonyesho  ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)yatakayoanza  hivi karibu jijini Dares salaam,Vodacom Tanzania ndiyo wadhamini wakuu wa Mawasiliano kwa vyombo vya habari katika kipindi chote cha Maonyesho hayo,Kulia Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo na Biashara Tanzania(Tan Trade)Bw.Samwel Mvingira.
Baadhi ya waandishi wa habari na maofisa wa Vodacom Tanzania wakifatilia mkutano wa Vodacom Tanzania kujitangaza rasmi kuwa wadhamini wakuu wa Mawasiliano na matangazo kwa vyombo vya habari katika kipindi chote cha Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa (sabasaba)yatakayoanza  hivi karibu jijini Dares salaam.
--
 *       Vodacom Kuendesha matangazo kwa Vyombo vya Habari katika kipindi chote cha Maonyesho.

*       Kampuni imetambuliwa kutokana na kutoa huduma na bidhaa rahisi na nafuu.
--
Dar es Salaam, 21 Juni 2012, 
Kampuni ya simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania leo imeingia katika ubia na Mamlaka ya Maendeleo na Biashata Tanzania (TanTrade) kama mdhamini maalum katika sekta ya mawasiliano kwenye maonyesho ya Kimataifa ya biashara Dar es Salaam.

Vodacom Tanzania itaendesha matangazo na vyombo vya habari kabla na baada ya maonyesho ndani ya siku kumi za maonyesho hayo ya kibiashara ambayo yataanza tarehe 30 ya mwezi juni.

Ushirikiano huu umekuja wakati ambapo sekta ya mawasiliano imekuwa na changamoto tangu mfumo wa kimaisha ya Kijamaa.  Ambapo watanzania wanatumia huduma ya simu kama njia ya kubadilishana mawazo katika ngazi ya familia na shuguli za kiofisi.
Vodacom Tanzania imeingia katika ushirikiano huu huku imafanikio  yake katika sekta ya mawasiliano ndani ya nchini Tanzania. Kampuni imekuwa ikitambulika kwa kupiga hatua zaidi katika kuhakikisha kuwa wateja  wanatumia simu  sio tu katika mawasiliano bali hata katika huduma za kifedha.

"Tumegundua hili na ndio maana tukaleta huduma ya kuamisha fedha ya Vodacom M- PESA, hivi sasa huduma hii imekuwa ni ya msingi kwa Watanzania walio wengi kutokana na huduma mbalimbali wanazopata kama kufanya malipo mbalimbali na kuhamisha fedha kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine" alibainisha Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza.

Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa Vodacom Tanzania inajitahidi kutoa huduma na bidhaa ambazo ni rahisi na nafuu kwa wateja wote nchini.Katika maboresho ya hivi karibuni, Vodacom Tanzania imezindua huduma mbalimbali ambazo ni maalum kwa vijana ikiwemo kampeni ya wajanja na Wajanja internet, huduma ambazo zinatoa nafasi  kwa vijana kupata huduma na bidhaa nafuu kutoka Vodacom alisema  Rene.

Vodacom Tanzania imewekeza kwa kiasi kikubwa katika maendeleo na maboresho ya miundombinu, kupitia hili kampuni inatarajia kuboresha ubora wa huduma na bidhaa zinazotolewa kwa wateja, ambapo sasa wataweza kumudu gharama za huduma na bidhaa hasa kwa vijana ili kuongeza watumiaji wa huduma na hadhi ya Kampuni..

Maonyesho ya kimataifa ya Dar es salaam Maarufu kama sabasaba, Ni maonesho ya kibiashara yanayoongoza Tanzania Maonyesho hayo yanayofanyika kwa siku kumi huvutia wageni zaidi ya 350000 na kujenga mahusiano na maingiliano baina ya watoa huduma na wateja wao na kutoa fursa kwa wateja kuangalia na kulinganisha ubora wa bidhaa.

Mwisho.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA