![]() |
Mustafa Hassanali Kuzindua UHURU collection Africa
Fashion Week
Precision Air, kumpeleka
Mustafa Hassanali to Afrika Kusini
Ni kwa mara ya Nane kwa
Mustafa Hassanali kufanya maonyesho in Afrika kusini.
Ikiwa Tanzania inasherehekea miaka 50 ya UHURU, mbunifu
wa kiafrika Mustafa
Hassanali’s,
atazindua “UHURU” collection ambayo alivutiwa na muonekano wa bendera ya taifa
kama iliyopeperushwa Mt Kilimanjaro tarehe 9
Desember 1961 AFI Afrika Fashion Week iliyopo Johannesburg Afrika Kusini.
“Mkusanyiko huo wa mavazi
umehusisha maliasili ya Tanzania, Ambao watu wake ni wenye
ukaurimu , nchi yenye utajiri wa maliasili za taifa na pia ni nchi iliyojengeka na misingi
aloiweka Baba wa taifa, Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere” alisema Mustafa Hassanali
Mkusanyiko huo wa mavazi
umepewa jina la UHURU. Na pia haupo tu
kusheherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bali uhuru huo kuonyesha
uwito, ubunifu na utamaduni.
Kwa kuwa taifa moja, Mkusanyiko huo wa mavazi utaonyesha Amani na utengenezaji wa
mavazi hayo yataielezea Tanzania kiundani kupitia mbunifu
wake kutoka Tanzania Mustafa Hassanali.
Safari ya Mustafa
Hassanali ya Afrika kusini imedhaminiwa na Precision Air, Shirika la ndege lenye
ukuaji mkubwa Tanzania ambalo kwa
sasa linafanya misafara
yake mara 5 kwa wiki kwa misafara ya
Johannesburg.
“Tunafarijika kuwa na
ushirika na Mustafa Hassanali, ambae atafanya maonyesho ya mkusanyiko wake wa mavazi kwa mara ya
nane Afrika kusini. Muungano wetu mpya unaangalia kutangaza biashara,utalii na
utamaduni uliopo kati ya Tanzania na Afrika Kusini.
alisema Afisa uhusiano wa Precision
air Annette Nkini.
Ikiwa ni mara ya kwanza
tena kwa Mustafa Hassanali, Atakuwa ni mbunifu pekee ambae atasherehekea miaka
50 ya uhuru wa Tanzanian nje ya Tanzania kwa kufanya ufunguzi wa
mkusanyiko wake wa Mavazi Afrika kusini.
“Maonyesho ya UHURU
collection yatakuwa ni maonyesho yangu ya pili AFI Africa Fashion Week na ya
nane kwa jamuhuri ya Afrika kusini, Itakayokuza mahusiano ya pande mbili kati ya
Tanzania na
Afrika Kusini.” Aliongeza Hassanali
AFI Africa Fashion week
inamilikiwa na African Fashion Internationals Dr Precious Moloi,
itakayofanyika Sandton Convention
Centre kuanzia tarehe 20-22
October. Mustafa Hassanali ndo mbunifu pekee kutoka Tanzania aliealikwa katika wiki ya
kujivunia na atafanya maonyesho yake
tarehe 22 October saa 10 jioni
KUHUSU MUSTAFA
HASSANALI
Mustafa Hassanali ni mbunifu mjasiriamali
anaeamini katika ‘daima sitashindwa’ huku akitumia kipaji chake na ubunifu wake
wa mavazi katika kuleta maisha bora ya sasa na ya baadae.
Kazi za mbunifu Mustafa zimekuwa
zikithaminika na kuonyeshwa kimataifa, ambapo Mustafa alifanikiwa kuonyesha
ubunifu wake katika nchi kama Angola ‘Angola Fashion Business’, FAFA (Festival
of African Fashion and Arts in Kenya), Kameruni, Wiki ya Mitindo India 2009,
Naomi Campbell’s fashion for relief 2009, Arise Africa Fashion Week 2009, Wiki
ya mavazi Durban & Cape town, Vukani Fashion Awards Pretoria, Miss Ethiopia
Beauty Pageant, Mediterranean Fashion Festival, Sicily, Italia, M’net Face of
Africa, Msumbiji, Uganda, na Wiki ya Mitindo Kenya, ambayo kwa pamoja yamemletea
heshima kubwa, ndani na nje ya nchi.
Ukikutana na Mustafa Hassanali ndipo utajua uwezo wake utokanao na
kazi zake,yeye kama yeye anajiamini katika kila anachokitengeneza na anatumia
karama na ubunifu wake kutengeneza kilicho bora leo na hata kesho,hasa katika
swala zima la mavazi, kwasababu kila akifanyacho hutoka moyoni. Mustafa ni
Fashionista wa kweli ndani na nnje
Kwa habari zaidi tembelea tovuti www.mustafahassanali.net
KUHUSU
PRECISION AIR
Shirika la
ndege Precision iimefungua matawi
yake mapya Johannesburg na
Hahaya-Comoros miezi miwili ilopita, tarehe 7th Octoba ilianza kuuza share zake
katika Initial Public Offering (IPO) na
ikitarajia kukuza Dolla za
kimarekani milioni 20 kwa ufungwaji
wa IPO tarehe 28th October.
Precision
Air ilitambuliwa na African Airlines Association (AFRAA) na
Best Scheduled Domestic
Airline kama shirika la ndege la mwaka 2010 kutoka Tanzania katika Tanzania Society of Travel Agents
(TASOTA) Awards .
Shirika hili la ndege
linamtandao mkubwa nnchini ikiwemo;
Dar es Salaam, Kilimanjaro, Zanzibar, Mwanza, Bukoba, Kigoma, Tabora,
Musoma, Shinyanga, Mtwara. Ukiachana na safari za mikoani shirika hili lina
safari zake pia Nairobi, Mombasa, Entebbe, na
kwasasa Hahaya na Johannesburg.
|
Friday, October 14, 2011

0 comments:
Post a Comment