



 |
Jana
majira ya saa kumi na dakika kadhaa jioni jeshi la polisi mkoani
Mwanza limefanikiwa kuwatia nguvuni watu wanne wanaotuhumiwa kwa
kufanya ujambazi wakiwa na bunduki moja aina ya smg na bastola mbili
moja ikiwa na risasi 12 na na ya pili ikiwa na risasi 2.Kwa
mujibu wa kamanda wa jeshi la polisi Mwanza Simon Sirro amesema kuwa
watu hao wamekematwa katika eneo la mtaa wa libert jirani na benki ya
NMB wakiwa kwenye harakati za safari kuelekea Nyegezi ambako walipanga
kwenda kufanya uvamizi kwenye duka moja.
Awali majambazi hayo yalivamia bar moja eneo la kilimahewa na kuwalaza
watu chini kisha kupora mali zao na kuiba bastola ya mteja mmoja.
Majambazi hayo yaliyokuwa katika gari dogo yalipostukia kuwa
yanafuatiliwa yalianza kufyatua risasi hovyo hali iliyosababisha
shughuli za biashara kwenye eneo la tukio kusimama kwa muda.
Raia wema ndiyo waliofanikisha kukamatwa kwa majambazi hao kwa kutoa
taarifa kwa jeshi la polisi ambao nao bila ajizi walifuatilia nyendo za
majambazi hao na hatimaye kufanikiwa kuwatia nguvuni.Wawili
kati ya majambazi hayo manne hali zao ni mbaya na wamepelekwa
hospitali ya Rufaa Bugando, mmoja katwangwa risasi mguuni na takoni ile
hali mwingine sugu anayetambulika kwa jina maarufu 'Askofu' akiwa
amevunjika mguu kabisa kwa kutwangwa risasi wakati alipojaribu
kuitoroka mikono
|
"Watu
wanatafuta fedha kwa njia zisizo halali kwa kutumia nguvu na hata
kufanya mauaji ili wapate fedha kwaajili ya sikuu ya pasaka, napenda
kuwatahadhalisha wote waliopanga kuingia Mwanza kufanya uhalifu kuwa
waondoke wakiwa wameaga makwao kwani hawatatoka wakiwa salama" amesema
kamanda Sirro.
Jeshi
la polisi mwanza linaendelea kufanya uchunguzi zaidi juu ya tukio zima
ambamba na kuwahoji watuhumiwa wote wanne wa mkasa huo.
0 comments:
Post a Comment