TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, April 6, 2011

Idadi ya Waliofariki dunia Loliondo yafikia 78

5:37 PM
Mwili wa mmoja kati ya waliopoteza maisha huko Loliondo.

Na Neville Meena na Mussa Juma, Samunge

IDADI ya watu waliopoteza maisha wakienda kupata tiba ya magonjwa sugu kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapila katika Kijiji cha Samunge, Loliondo Wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha imefikia 78.Habari ambazo Gazeti la Mwananchi limezipata na kuthibitishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Dominick Lusasi zinasema idadi ya vifo hivyo ni ile iliyorekodiwa kuanzia Machi 11, mwaka huu.

"Kati ya Machi 11, mwaka huu tulipoanza kuchukua rekodi za waliokufa na Machi 29, watu 74 walikuwa wamethibitishwa kufariki dunia, lakini hivi karibuni nilipata taarifa kwamba watu wengine wanne wamefariki," alisema Lusasi.

Hata hivyo, idadi hiyo inaweza kuwa ndogo kuliko uhalisia kwani upo uwezekano mkubwa kwamba wapo waliofariki dunia na vifo vyao havikurekodiwa tangu watu walipoanza kufurika Samunge mwishoni wa Januari ,mwaka huu hadi Machi 11, 2011 utunzaji wa kumbukumbu ulipoanza.
Habari hii ni kwa hisani ya
Mwananchi.co.tz
 

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA