Mwili wa mmoja kati ya waliopoteza maisha huko Loliondo.
Na Neville Meena na Mussa Juma, Samunge
IDADI ya watu waliopoteza maisha wakienda kupata tiba ya magonjwa sugu
kwa Mchungaji Ambilikile Mwasapila katika Kijiji cha Samunge, Loliondo
Wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha imefikia 78.Habari ambazo Gazeti la
Mwananchi limezipata na kuthibitishwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Dominick Lusasi zinasema idadi ya
vifo hivyo ni ile iliyorekodiwa kuanzia Machi 11, mwaka huu.
"Kati
ya Machi 11, mwaka huu tulipoanza kuchukua rekodi za waliokufa na Machi
29, watu 74 walikuwa wamethibitishwa kufariki dunia, lakini hivi
karibuni nilipata taarifa kwamba watu wengine wanne wamefariki," alisema
Lusasi.
Hata
hivyo, idadi hiyo inaweza kuwa ndogo kuliko uhalisia kwani upo
uwezekano mkubwa kwamba wapo waliofariki dunia na vifo vyao
havikurekodiwa tangu watu walipoanza kufurika Samunge mwishoni wa
Januari ,mwaka huu hadi Machi 11, 2011 utunzaji wa kumbukumbu ulipoanza.
|
0 comments:
Post a Comment