Askari wanaomtii Kanali Gaddafi mjini Misrata
Majeshi yanayoiunga mkono serikali yamezidi
kuwashambulia waasi nchini Libya, nahivyo kuwalazimu kurejea nyuma
katika mji wa Bin Jawad.
Mapigano hayo mapya yameibuka baada ya wajumbe
kutoka nchi mbalimbali kukutana mjini London kwenye mkutano wa kujadili
mipango ya usoni ya Libya.
Awali Rais wa Marekani Obama alijitetea kwa
kufanya uamuzi wa kuidhinisha harakati za kijeshi kwa mara ya kwanza
tangu aingie madarakani, akisistiza Marekani imejihusisha kwa kiwango
kidogo.
Lakini pia alisema kumwondoa Kanali Gaddafi kwa nguvu ni kosa.
Majeshi yanayompinga Kanali Gaddafi yamesogea
sana upande wa magharibi kutoka kwenye ngome yao ya Benghazi katika siku
za hivi karibuni- wakisaidiwa sana na mashambulio ya anga ya kimataifa-
yakiteka idadi kadhaa za jamii za kipwani na mitambo muhimu ya mafuta,
ikiwemo Ras Lanuf, Brega, Uqayla na Bin Jawad. |
0 comments:
Post a Comment