TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, March 30, 2011

Majeshi ya Gaddafi yawazidi nguvu waasi

3:10 PM
Askari wanaomtii Kanali Gaddafi mjini Misrata
Majeshi yanayoiunga mkono serikali yamezidi kuwashambulia waasi nchini Libya, nahivyo kuwalazimu kurejea nyuma katika mji wa Bin Jawad.
Mapigano hayo mapya yameibuka baada ya wajumbe kutoka nchi mbalimbali kukutana mjini London kwenye mkutano wa kujadili mipango ya usoni ya Libya.
Awali Rais wa Marekani Obama alijitetea kwa kufanya uamuzi wa kuidhinisha harakati za kijeshi kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani, akisistiza Marekani imejihusisha kwa kiwango kidogo.
Lakini pia alisema kumwondoa Kanali Gaddafi kwa nguvu ni kosa.
Majeshi yanayompinga Kanali Gaddafi yamesogea sana upande wa magharibi kutoka kwenye ngome yao ya Benghazi katika siku za hivi karibuni- wakisaidiwa sana na mashambulio ya anga ya kimataifa- yakiteka idadi kadhaa za jamii za kipwani na mitambo muhimu ya mafuta, ikiwemo Ras Lanuf, Brega, Uqayla na Bin Jawad.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA