TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, January 29, 2011

Tour la Steven Kanumba Huko HollyWood na BeverlyHills

8:14 PM

Kwa kumalizia ziara yangu ya kutembelea hollywood nimetembelea ule ukumbi maarufu wa michezo mbalimbali hasahasa basket ball kutizama mchezo wa HOCKY unaopendwa sana hapa USA,Kikubwa kilichonifanya nije hapa si a kwa ajili ya show yake ya THIS IS IT,lakini pia humu ndipo mwili wake ulipoagwa mara baada ya kifo chake,Pia ukumbi huu ndio timu kubwa kama Lakers na LA KINGS hucheza mechi zake..nami nikaona ni vyema nije niione jinsi ulivyo unaitwa STAPLES CENTER.
nikitazama logo ya kampuni hii

Mitaa hii ya hollywood usiku na mchana imejaa wasanii mbalimbali ambao hawana tabu kupiga nao picha kama hivi
Mafuvu yaliyomo madame tussaunds yakutengenezwa ambayo pia ndiyo hutumika kwa shooting,mafuvu yanayoonekana katika movie huwa sio halisi,inasemekana yanatengenezwa kwa unga unaotengeneza mishumaa alafu wanayapaka rangi na kuwa hivyo unavyoona.

Kupitia movie ya Harry Potter niliuliza maswali mengi kitu kilichopelekea msimamizi wangu kunionesha kwa vitendo jinsi kile kifimbo kilivyokuwa kinabadilishwa hakika nilipata elimu sawia ambayo nisingeipata pengine zaidi ya hapa.

Harry potter,gari yake na mhusika mwenyewe,katika movie gari inaonekana inapaa lakini wapi ilikuwa hapo hapo tu,hayo mambo ya special effect.

Mr.Jingo na mimi uwanjani

Terminator ya Anord.

Hollywood walk of fame penye alama mbalimbali za mastaa akiwemo Michael Jackson.
---
BAADHI YA MASWALI NILIYOULIZA WARNER BROTHER STUDIO&UNIVERSAL STUDIOS:-

1.Je hollywood mnachukua mda gani kushoot filamu,JIBU:-miezi 2 mpaka 3.,,editing nayo inategemea na aina ya movie zipo zinazochukua miezi 2,na zingine 6,maana kuna vitu vingi vya kuangalia ikiwemo special effect,sound,nk.


2.Je mnapataje waigizaji hasa wapya?JIBU:-Tuna tangaza na watu wanakuja katika interview lakini pia kuna makampuni yanayohusika na casting wakati mwingine tunawapa hali halisi ya watu tunaowaitaji alafu wao hutafuta na kutuletea.


3.Mtu kama anataka kucheza movie hollywood kampuni yoyote afanyaje?JIBU:-Akisikia matangazo afanye hima kujaribu bahati yake au pia anaweza kujisajili katika hizo kampuni za casting,au anaweza kututumia Head shot(picha zake full na ya karibu) na CV na mawasiliano yake.


4.Mbona mimi mwaka 2007 niliacha hapa headshot,cv na mawasiliano yangu lakini sijawai itwa?JIBU:-Kila mtu ana bahati yake na wanaotuma hivyo vitu ni wengi kulingana na idadi inayoitajika pia sio lazima ukituma hivyo lazima uchukuliwe wewe,yoyote anawezachukuliwa kulingana na director anataka nini,lakini pia sio wote hupitia njia hizi,hollywood kila mtu kaingia kwa njia yake..tizama mtoto wa will smith katika ile movie ya Karate Kid kapata connection kupitia baba yake,kuwa na connection nalo ni muhimu,Samuel Jackson kasota sana kabla ya kuwa hapo alipo ameigiza sana katika stage lakini sasa ni star wa dunia.


5.Movie ikishakamilika inapitia hatua zipi mpaka kuwa katika DVD?JIBU:-Hupelekwa sinema huko ndiko pesa nyingi hutengenezwa,hukaa huko miezi 2 na zaidi kama movie imetokea kupendwa dunia nzima,baada ya hapo hupelekwa katika tv kuoneshwa ambapo hapo station husika hulipia kuonesha movie hiyo hapo napo pesa ingine hutengenezwa,mwisho kabisa ndio huwekwa katika DVD kuuzwa,dvd huwa hatua ya mwisho japo pia PIRATES nao wanaharibu soko maana unaweza kuta movie bado iko theatre lakini nchi fulani zina dvd zake.

NAISHIA HAPA MENGINE YANABAKI KWA FAIDA YANGU.
By
Steven Kanumba

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA