TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, January 29, 2011

Polisi na waandamanaji wapambana Misri

2:08 PM

Polisi wamepambana na maelfu ya waandamanaji kwenye mji mkuu wa Misri, Cairo, baada ya sala ya Ijumaa wakitaka Rais Hosni Mubarak ajiuzulu.

Polisi walirusha mabomu ya machozi na kutumia mizinga ya maji kusambaza watu, waliokuwa wakirusha mawe.

Watu hao pia waliandamana katika miji ya Suez na Alexandria.


Serikali ilisema iko tayari kwa mjadala, lakini pia imeonya kuchukua "hatua madhubuti".

Mawasiliano ya kupata huduma za wavuti na simu za mkononi yamekatizwa.

Kulikuwa na ripoti za kuanza upya kwa mapigano, pamoja na viongozi wa upinzani kukamatwa.

Pia kulikuwa na hatua kali za kinidhamu dhidi ya kundi la kiislamu lililopogwa marufuku, the Muslim Brotherhood, baada ya kusema itaunga mkono maandamano hayo siku ya Ijumaa.

Siku ya Alhamis,

Takriban watu saba wameuawa na takriban 1,000 wamekamatwa tangu maandamanao hayo yalipoanza.

Maandamano hayo yameanza baada ya kuwepo ghasia Tunisia, yaliyosababisha kukimbia kwa Rais Zine al-Abidine Ben Ali.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA