Hii ndio ilikuwa safari ya mwisho ya mpiga drums wa Band ya Twanga Pepeta Abuu Semuhando enzi hizo akifahamika kama Baba Diana,Baba Sharifa ama Baba Zaituni.Mazishi ya Baba Diana yalifanyika nyumbani kwake katika kijiji cha Kibanda Muheza mkoani Tanga.Mamia ya wanamuziki na Wadau mbalimbali wa muziki walijitokeza kwenda kumzika mwanamuziki huyo aliyefariki kwa ajali ya kugongwa na gari akiwa na pikipiki yake.Mimi na wafanyakazi wenzangu wa RJ Company nawapa pole familia ya Semuhando na kampuni ya ASET kwa kumpoteza mtu muhimu katika band.Mungu amuweke mahala pema peponi Amen
Mkuregenzi wa ASET Asha Baraka akipokea dua kabla ya kwenda kuzika
Asha Sharapova akilia kwa uchungu kwa kumpoteza kiongozi wake katika Band
Ilikuwa ni huzuni tupu katika kijiji cha Kibanda muheza
0 comments:
Post a Comment