Ni movie iliyowashirikisha baadhi ya watanzania na waingereza nchini Uingereza inayojulikana kwa jina la KINGKONG.Watanzania walioshiriki movie hii mwanzo walikuwa wanajishughulisha na sarakasi na sasa wamegeukia kwenye filamu mmoja anaitwa Hilal Majaliwa na mwenzake anajulikana kwa jina la Nasoro.Kwa dondoo nilizopewa na Hilal Majaliwa aliyenitumia picha hizi ameniambia movie hii imechukuwa takribani mwaka mmoja tangia ishutiwe na mpaka leo bado haijatoka ipo studio ikifanyiwa kazi.Malipo ambayo wamepewa ni mazuri ukilinganisha na malipo ambayo wanalipwa wasanii wa kitanzania hapa nchini,Kwakweli hata ukiangalia picha utagundua movie hii imegharimu pesa nyingi maana hata location ni za kutengeneza
Hawa nyani sio nyani wenyewe kabisa ni nyani watu ambao wametengenezwa
Angalia jinsi nyani walivyokaa tayari kwa picha
Nyani mkubwa akiwa amezungukwa na watu,Nyani kama huyu ni wa kutengeneza
Dada huyu ni mmoja wa waigizaji katika movie hii
Majaliwa akiwa na wenzake kwenye setting
Angalia hii location iliandaliwa kabisa,Ni vitu vinavyofanya filam zinakuwa za gharama kubwa maana kutengeneza location si kazi ndogo lakini tutafika tuu na sisi huko maana hata wao miaka hiyo walikuwa kama sisi
Watu wakiwa kwenye set
Kama nilivyosema filam hii ni mchanganyiko wa Waingereza na Watanzania
Nakuomba Mdau wangu Majaliwa unitumie na picha za vifaa mlivyofunga wakati mnarekodi na Production crew nzima ili wadau wengine waone production za nje zinavyokuwa
0 comments:
Post a Comment