TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, March 30, 2010

India yaanza kuchunguza visa vya uharamia

4:42 PM

Serikali ya India inachunguza ripoti kuwa maharamia wa Kisomali wameteka nyara mashua kadhaa za nchi hiyo na zaidi ya mabaharia mia moja.

Jeshi la wanamaji nchini humo limesema mabaharia wa meli moja iliyoachiliwa huru na maharamia wa Kisomali wamesema meli zingine nyingi bado zinashikiliwa na maharamia hao.

Ripoti zingine zinasema maharamia hao wanazuilia mashua za uvuvi pekee huku zingine zikidai kuwa ni meli ya mizigo zilizokuwa zikielekea eneo la Ghuba.

Habari hizo zimetolewa baada ya jeshi la wanamaji nchini Ushelisheli na lile la muungano wa Ulaya linaloshika doria katika pwani ya Somalia kuwanasa maharamia katika meli moja iliyokuwa imetekwa nyara, kabla ya kuwakomboa mabaharia wake.


1 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA