TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, January 27, 2010

Marekani yakosoa utawala wa Nigeria

2:14 PM

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hillary Clinton amekosoa vikali utawala wa Nigeria kwa kutowajibikia majukumu yake vilivyo.

Bi Clinton amesema hali mbaya ya maisha nchini Nigeria imesababisha wananchi wengi na hasa vijana kuhisi kwamba wametengwa na sasa wamekuwa walengwa wa makundi ya kigaidi ambayo yanawasajili na kuanza kuwapa mafunzo ya itikadi kali.

Amezungumzia ongezeko la machafuko na uasi nchini Nigeria na kisa cha raia wa Nigeria Umar Farouk Abdulmutallab, ambaye anadaiwa kuhusika katika jaribio la kuidungua ndege katika anga za marekani mnamo siku ya krismasi.

Bi Clinton na Rais Barack Obama wameweka mbele kampeini ya kuwezesha utawala bora barani Afrika katika agenda yao.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA