Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, aliyasema hayo jana wakati akiongea na wafanyakazi wa Mamlaka ya majisafi na majitaka mjini Moshi (Muwsa) katika ziara yake ya siku mbili mkoani Kilimanjaro.
Alisema serikali kupitia wizara yake na wafadhili mbali mbali wamekuwa wakitekeleza azma ya kuwapatia maji safi na salama wananchi wa vijijini ili kuondokana na adha ya upatikanaji wa maji na kuondokana na umasikini.
Mwandosya alitoa wito kwa mamlaka hiyo kuanzisha ushirikiano wa kutunza vyanzo vya maji na misitu iliyopo katika hifadhi ya mlima Kilimanjaro na kuwa na vyanzo endelevu vya maji ambapo pia aliagiza mamlaka hiyo kusimamia kikamilifu kazi zinazofanywa na wahandisi wa maji kwa kufuatilia taarifa za utekelezaji wa programu ya maji vijijini.
Mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na maji taka mjini Moshi, Antony Kassonta, alisema mamlaka yake imepokea Sh. 925,552,124 kwa ajili ya utekelezaji wa programu ya maendeleo ya usambazaji wa maji katika wilaya za Mwanga, Same na Himo Wilaya ya Moshi vijijini.
Alisema programu ya maendeleo ya sekta ya maji katika mji wa Same utahusisha vijiji 37 katika wilaya za Mwanga, Same na Korogwe na kwamba mradi huo utahusisha utoaji wa maji kutoka bwawa la Nyumba ya Mungu.
0 comments:
Post a Comment