TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, September 29, 2009

Vifo vyaongezeka nchini Guinea

8:41 AM

Takriban watu 87 wameuawa baada ya majeshi ya Guinea kuwafyatulia risasi kundi kubwa la waandamanaji kwenye mji mkuu wa Conakry.

Kutokana na chanzo kimoja cha polisi, idadi ya watu 58 walioripotiwa kufariki dunia hapo awali imeongezeka kufikia 30.

Inakadiriwa watu 50,000 waliandamana kumpinga Kapteni Moussa Dadis Camara aliyechukua madaraka nchini humo mwaka jana.

Kapteni Camara alitwaa madaraka baada ya kufanya mapinduzi yasiyohusisha umwagikaji damu.

Maandamano hayo yaliibuka baada ya Rais Camara kubadilisha msimamo wake wa kutogombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Januari.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA