
Mkuu wa tume ya kupambana na rushwa nchini Kenya ambaye uteuzi wake ulikuwa umepingwa na watu wengi wa nchi hiyo, hatimaye amejiuzulu ikiwa ni wiki chache baada ya kuteuliwa na rais.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Uingereza la Reuters, Aaron Ringera amesema anajiuzulu kwa manufaa ya nchi.
Rais Mwai Kibaki alikuwa anataka jaji huyo mstaafu kutumikia muhula wa pili akiwa mkuu wa tume ya kupambana na rushwa nchini humo maarufu Kenyan Anti-Corruption Commission.
Lakini mapema mwezi wa Septemba, Wabunge walisema uteuzi huo wa rais ni kinyume na sheria na waliukataa uteuzi huo.
Waandishi wa habari wanasema Bwana Ringera alikuwa akilaumiwa na Wakenya kwa kutofanya vya kutosha katika kupambana na rushwa.
Alikuwa akipokea mshahara mkubwa akiwa mtumishi wa serikali, wa shilingi za Kenya milioni 2.5 kwa mwezi, kuliko mshahara anaopata rais.
0 comments:
Post a Comment