
Na Boniface Meena
NAIBU katibu mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amesema ana sababu za msingi za kuamua kuuwania uenyekiti wa chama hicho, huku mwenyekiti wake Freeman Mbowe akimkaribisha katika kinyang'anyiro hicho.
Zitto, ambaye yuko nchini Ujerumani kikazi, aliiambia Mwananchi jana kwamba, ameamua kuingia katika kinyang’anyiro cha uenyekiti kupambana na Mbowe kwa lengo la kuandaa chama kuchukua dola.
Lakini Mbowe, ambaye uongozi wake umeifanya Chadema kuwa tishio kwa chama tawala na upinzani, alisema anamkaribisha mwanasiasa huyo kijana katika kuwania nafasi hiyo, akisema uamuzi huo ni haki ya kila mwanachama wa chama hicho kugombea nafasi yoyote kama ana sifa.
"Sina mengi ya kusema; kama alivyosema Dk Slaa (Willibrod) kila mwanachama anaruhusiwa kugombea nafasi yoyote, hivyo sina tatizo na Zitto kuwania nafasi hiyo," alisema Mbowe.
Zitto, ambaye ameibukia kuwa mwanasiasa maarufu mwenye uwezo wa kujenga hoja, alisema anatambua kazi nzuri ambayo Mbowe ameifanya katika chama, lakini akaongeza kuwa, uamuzi wa kupambana naye unalenga kukiandaa chama kuchukua dola katika chaguzi zijazo.
0 comments:
Post a Comment