Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba
(41).HOMA ya Uchaguzi Mkuu 2015 inazidi kupanda. Wapo baadhi ya wagombea
wa urais ambao tayari wameshatangaza nia hadharani lakini wengine
wanaendeleza harakati zao chini kwa chini.
Miongoni mwa makada ambao tayari wameonesha nia ya kutaka kugombea ni
pamoja na vijana, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba (40) na Naibu
Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba (41).
Mwigulu ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi mkoani Singida, amekuwa
na mvuto wa aina yake kisiasa huku akionekana kupendwa zaidi kutokana na
kujiwekea nembo yake kwenye mavazi anayovaa kwa kujifunga skafu ya
bendera ya taifa.

0 comments:
Post a Comment