TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, March 2, 2013

Rais kikwete afunguka kuhusu wachochezi wa kidini

11:12 AM


kikwete
RAIS Jakaya Kikwete  amewaagiza polisi, wakuu wa mikoa na wa wilaya kutofanya ajizi kwenye suala la wachochezi wa kidini, bali wachukue hatua stahiki na kwa haraka ili kuendeleza amani ya nchi.

Kikwete alitoboa hayo kupitia hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa juzi kwa Taifa  kupitia vyombo vya habari Dar es Salaam.

“ Nimewakumbusha polisi na mamlaka husika kote nchini wasifanye ajizi kwenye matukio ya namna hiyo.

Wawachukulie hatua stahiki wale wote wanaohusika.  Nimewataka wazingatie msemo wa Kiswahili usemao ajizi nyumba ya njaa”, alisema.

Alisema kuwa wachochezi wa mifarakano  na chuki za kidini wasipodhibitiwa ipasavyo wataleta maafa kwa Watanzania wasiokuwa na hatia akiwataka wakuu wa wilaya na mikoa kutimiza ipasavyo wajibu wao kama walinzi wa amani.

Alisema wakati wote Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaochochea chuki za kidini, wanaodharau vitabu vitakatifu vya dini nyingine na wanaokejeli dini nyingine

Kuhusu matokeo mabovu ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, Rais Kikwete alitaka utafiti ufanyike ili kujua chanzo  na kusisitiza kwamba   bila utafiti wa kina kufanyika , tatizo hilo linaweza kuwa kubwa na kuligharimu taifa.

“Wanafunzi 397,132 walifanya mtihani huo na kati yao, waliofaulu ni 126,851 sawa na asilimia 34.5,  wanafunzi  240,903 ambao ni asilimia 65.5 hawakufaulu. Kwa ulinganifu, matokeo hayo ni mabaya kuliko matokeo mengine ya mtihani huo ya miaka ya hivi karibuni.

Ni suala muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu, hivyo lazima ukweli wake ujulikane kwa uhakika,”alisema Rais Kikwete na kuongeza:

“Matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012, yameshtua na kufadhaisha watu wengi nchini na kwa sababu stahiki kabisa.

Kwanza, kwamba kiwango cha kufaulu kimeporomoka sana, tena ghafla, kutoka asilimia 53.6 mwaka 2011 hadi asilimia 34.5 mwaka 2012.  Hili ni anguko la asilimia 19.1 ambalo, kwa kila hali, ni kubwa sana.”

Rais Kikwete alisema kuwa mambo hayo, ndiyo msingi wa uamuzi wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuamua kuunda Tume ya kuliangalia suala zima la mitihani ya mwaka 2012 na matokeo yake.
CHANZO MWANANCHI.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA