Matokeo ya mapema ya uchaguzi wa urais nchini Kenya yanaonyesha
Uhuru Kenyatta ameshinda na kuepuka raundi ya pili ya uchaguzi. Takwimu kutoka
tume ya uchaguzi zinasema Kenyatta ameshinda asilimia hamsini nukta tatu za kura
zote zilizopigwa.
Lakini tume ya uchaguzi itakagua hesabu hiyo kabla ya kutangaza matokeo
baadaye leo jumamosi, siku tano baada yawakenya kupiga kura.
Kenyatta anakabiliwa na mashtaka katika mahakama ya kimataifa ya ICC
kuhusiana na ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007.
Waandishi wa BBC wanasema iwapo Kenyatta atakabidhiwa ushindi katika raundi
ya kwanza, mpinzani wake waziri Mkuu Raila Odinga atakwenda mahakamani kupinga
matokeo hayo.
Tume ya uchaguzi itatangaza matokeo rasmi ya mshindi baadaye leo
Tume hiyo pia itatangaza mshindi wa uchaguzi huo na vile vile kama mshindi
huyo ametimiza masharti ya kikatiba ya kutangazwa kuwa rais wa nne wa Kenya.
Kamishna Yusuf Nzibo alitoa taarifa hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume
Isaack Hassan.
Vile vile mgombea huyo pia lazima awe ameshinda asilimia 25% katika nusu ya
County zote 47 nchini kenya.
Awali Waziri Mkuu Raila Odinga alikuwa amewaalika waandishi wa habari
nyumbani kwake kwa mkutano maalum ili azungumzie maswala ya matokeo ya urais
lakini baadaye mkutano huo uliakhirishwa hadi siku ya Jumamosi , baada ya tume
ya uchaguzi kutoa tangazo lake la mwisho. |
0 comments:
Post a Comment