TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, June 26, 2012

John Mnyika:- Mrejesho wa Bungeni leo, Juni 26, 2012

6:02 PM
Mosi, nimeuliza swali la nyongeza la kutaka ofisi ya Rais iwawajibishe watendaji waliozembea kuingiza maelezo na vielelezo vya waajiriwa wapya na waliopandishwa vyeo na kusababisha wachelewe kulipwa mishahara na kulimbikiza madai hali inayochochea migomo na migogoro kati ya wafanyakazi na serikali.

Pili, nimeomba muongozo baada ya kauli ya Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuhusu kushuka kwa bei ya samaki aina ya Sangara kwenye ukanda wa ziwa Victoria kwa kuwa kauli hiyo ina mambo yenye kuzua mjadala kinyume na kanuni 49 (2) hivyo nikataka muongozo wa spika atumie kanuni ya 116 kuwezesha kamati ya bunge ya mifugo na maji kujadili kauli hiyo na kuleta taarifa bungeni wabunge tuweze kutimiza wajibu wa kuisimamia serikali.

Aidha, nilitaka muongozo kwa kanuni 64 (1) (c) na 116 kuhusu mgomo wa madaktari, suala ambalo nitamwandikia spika na bunge kusuluhisha kwa mujibu wa ibara 63 (2).

John John Mnyika,
Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA)
26 Juni, 2012

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA