TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, May 30, 2012

Iddi Simba Kufikishwa Mahakamani Leo; Tafsiri Yangu

2:06 AM
Na maggid mjengwa
Nimeiona habari kubwa kwenye ITV usiku wa leo; Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Bw. Iddi Simba amefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.  Ni Iddi Simba ambaye alilazimika kujiuzuru uwaziri kwa kashfa ya sukari. Ni Iddi Simba ambaye huko nyuma aliipigania sana sera ya Uzawa.

Na kadhia iliyomkumba sasa  inahusu kafsha ya UDA. Ni  lililokuwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam. Iddi Simba amesomewa mashtaka 8 ikituhumiwa   kudanganya, kughushi na kulitia hasara ya shilingi milioni  320 Shirika la Usafiri Dar es Salaam ( UDA).

Tafsiri yangu;
Huu ni mwendelezo wa mwanzo uliotiliwa mashaka. Kuna watakaoanza kuamini, kuwa zama za kulindana zimeanza kufikia ukingoni. 

Iddi Simba ni kigogo. Ni Mzee wa Dar es Salaam. Ni Mwenyekiti wa Wazee wa Dar es Salaam. Leo amefikishwa kwenye Mahakama ya katikati ya Jiji la Dar. Bila shaka, kuna ambao hawakuamini kumwona Idi Simba kwenye runinga akikalia kwenye benchi la Mahakamani. 

Naam, tunaziona ishara la wimbi kubwa linalokuja, si dogo hata kidogo. Yumkini naye anasafisha njia ya wengine kufuatia. Na tusubiri tuone.
  

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA