Ikiwa kweli Mutassim Gaddafi atakuwa amekamatwa, hii itakuwa habri njema kwa baraza la mpito na pigo kwa makundi yaliosalia yanayo mtii kanali Gaddafi.
Inadaiwa kuwa wanajeshi waliokuwa wakipigana na wale wa baraza la NTC mjini Sirte alipozaliwa Kanali Gaddafi wamekuwa wakimlinda Mutassim.
Ikiwe ni kweli amekamatwa, Mutassim atakuwa wa mtu wa kwanza wa wa jamaa ya Gaddafi kushikwa.
Mke wa kanali Gaddafi na watoto wake wakike wapo nchini Algeria na kaka yake Saif al Islam anadaiwa kuwa mafichoni mjini Bani Walid.
Raia wengi wa Libya wanaounga mapinduzi haya wanahamu kuona kanali Gaddafi ameshikwa akiwa hai.
0 comments:
Post a Comment