TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Sunday, March 6, 2011

Wakanusha kudhibiti miji Libya

11:34 PM

Miji minne ya nchini Libya ambayo majeshi yanayomtii Kanali Muammar Gaddafi yalidai kuidhibiti imesalia mikononi mwa wapinzani, kwa mujibu wa watu waliopo katika maeneo hayo.
Libya
Mapigano imeendelea Libya
Tobruk na Ras Lanuf, imesalia mikononi mwa waandamanaji, walisema waandishi wa habari wa BBC.
Majeshi yanayompinga Kanali Gaddafi, yanashikilia miji ya Misrata na Zawiya, kwa mujibu wa habari za wapinzani na wakazi wa huko.
Lakini Misrata na Ras Lanuf ilishambuliwa siku ya Jumapili, na pia mapigano yameripotiwa katika mji mdogo wa Bin Jawad.
Libya
Wapinzani
Mjini Tripoli, maafisa walisema milio ya bunduki iliyosikika saa za alfajiri ilikuwa ya wapinzani wakisherekea kudhibiti miji.
Watu wengi awali walidhani milio hiyo ilikuwa ni mapigano kati ya majeshi ya wanaomtii na wanaompiga Kanali Gaddafi, na pia kuna tetesi kuwa hiyo milio ya buduki ya kusherekea ilikuwa kisingizio cha kufunika mapigano.
Tripoli imekuwa ngome kuu ya Kanali Gaddafi, wakati akijitahidi kurejesha udhibiti wa nchi kutoka kwa wanaompinga, ambao wamechukua eneo kubwa la upande wa mashariki, na pia katika miji ya karibu na Tripoli, upande wa magharibi.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA