TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, March 29, 2011

DAWA YA BABU HAINA MADHARA. SERIKALI

8:15 AM
Taarifa ya habari iliyosomwa saa saba mchana wa leo kupitia TBC , imetamka kuwa, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (?Serikali au Sehemu ya Serikali?) imetoa ripoti kuhusu tiba inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa La Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapila* al maaruf, "Babu" huko kijijini Samunge, Loliondo wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha na kusema, "dawa hiyo haina madhara kwa binadamu".

Ripoti hiyo inafuatia utafiti uliofanywa na timu ya wataalamu toka Mamlaka ya Dawa na Chakula, TFDA, wakishirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binaadamu, NIMR, na Kitengo cha Utafiti wa Dawa za Asili cha Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam, kwamba baada ya uchunguzi wa dawa na kipimo kinachotolewa na "Babu" (kikombe cha Babu) haina madhara kwa binadamu.

Bofya kifute cha play kusikiliza taarifa ya Habari hiyo.
*Usahihi wa jina la Mchungaji
Kumekuwapo upotoshaji wa jina la Mchungaji husika. Awali, aliitwa Mchungaji (mstaafu) Ambilikile Mwasapile. Wengine wakamwita Ambilikile Mwaisapile. Wapo wanaomwita Ambilikile Mwasapila na wengine wakamwita Ambikile Masapile. Uongozi wa Kanisa la KKKT umetoa ufafanuzi wa jina lake halisi na kusema ni Mchungaji (mstaafu) Ambilikile Masapila. (credit  ya ufafanuzi wa jina New Habari)



0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA