| waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hadji hussein Mponda amesema
serikali imemsimamisha kwa muda tiba ya mchungaji mstaafu wa kanisa la
KKKT Ambikile Mwasapile anaedaiwa kutibu magonjwa mbalimbali ikiwemo
ukimwi kwa gharama ya shilingi mia tano
Katika hatua nyingine Serikali imepokea pikipiki 30 kati ya 400
ilizoagiza kwa ajili ya kubebea wagonjwa zitakazotumika kwa ajili ya
kusafirisha wagonjwa wa rufaa kati ya zahanati na vituo vya afya.
Akizungumza jijini Dar es salaam leo waziri amesema pikipikipi hizo
ambazo kila moja ina thamani ya dolla 5900 zitarahisisha kusafirisha
wajawazito kutoka kituo kimoja hadi kingine
Kwa mujibu wa waziri, pikipiki hizo zitapelekwa katika mikoa ya pwani,
Morogoro, Rukwa, Mbeya na Dodoma.
Aidha waziri Mponda amesema pikipiki hizo zitakuwa na manufaa kwa nchi
yetu kwa kuwa tayari kuna nchi nyingine zimeshaanza kutumia ambazo ni
Kenya, Malawi, Afrika kusini, Sudan kusini, Ethiopia na Guinea.
|
0 comments:
Post a Comment