Raia watano wa Somalia waliopatikana
na hatia ya kutaka kuteka meli ya jeshi la majini ya marekani
waliodhania ni meli ya kibiashara wamehukumiwa adhabu ya kifungo cha
maisha jela.
Watu hao wanaosadikiwa kuwa
maharamia wamepatikana na hatia mwezi Novemba kwa kujaribu kuteka meli
ijulikanayo kama USS Nicholas, meli iliyokuwa ikifanya doria kudhibiti
utekaji wa meli baharini.
Mawakili wa utetezi wamedai kuwa
wasomali hao walikuwa wametekwa na maharamia na kulazimishwa kufyatua
silaha zao dhidi meli hiyo ya Marekani katika shambulio lililofanyika
mwezi Aprili.
Waendesha mashitaka wamesema
Wasomali hao wanakuwa wa kwanza kuhukumiwa na mahakama ya Marekani kwa
kosa la uharamia tangu mwaka 1820.
|
0 comments:
Post a Comment