TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, February 19, 2011

NDULI NI UWANJA WA NDEGE AMBAO NI KILIO KWA TAIFA....

6:37 PM
WAKATI Taifa likiwa katika simanzi kubwa ya vifo vya watu zaidi ya 20 waliopoteza maisha katika tukio la mabomu kambi ya jeshi Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam ,hali ya usalama kwa viongozi na wasafiri wa anga wanaotumia uwanja wa Ndege wa Nduli Iringa ni mashakani na ni sawa na bomu jingine kwa Taifa mtandao huu umebaini .

Mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com na ule wa www.shwari.com umepata kutembelea uwanja huo wa Nduli kabla ya ziara mbali mbali za viongozi wa kitaifa na baada ya ziara hizo za viongozi na kushuhudia udanganyifu mkubwa ambao umekuwa ukifanywa na viongozi wa mkoa wa Iringa kwa viongozi hao katika harakati za kuficha aibu ya ubovu wa gari la zima moto katika kiwanja hicho cha Ndege .


Uchunguzi wa kina uliofanywa na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com umebaini kuwa gari linalotumika kwa sasa ambalo ni maalum kwa ajili ya uwanja huo wa Ndege Nduli ni gari aina ya Mazda lenye namba STH 69 34 ni gari la kizamani ambalo limekuwa si msaada wowote katika uwanja huo zaidi ya kusaidiwa na gari kubwa la kikosi cha Zimamoto katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.hapa

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA