TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, January 20, 2011

Ras Nas kufanya shoo Belleville, Oslo. 28 Januari

9:33 PM

Kiota cha maraha Belleville, Oslo, kitawaka moto mkali wakati Ras Nas na kikosi chake watakapofanya kweli Ijumaa tarehe 28 mwezi huu. Tumbuizo hili ni la kwanza mwaka huu kwa Ras Nas ambaye ameahidi kufanya shoo la kufa mtu. Safu ya wanamuziki safari hii inajumuisha mpiga sax mahiri toka Mozambique, Ivan Mazuze, mkaanga chipsi (drummer) Uriel Seri toka kwa Gbagbo, Ivory Coast, na mkun'guta besi Aristide Milongo tokea Congo Brazzaville. Wengine ni Dag Pierre, gitaa toka Sweden na Thor Erik mpiga kinanda toka Norway. Mwanamuziki Ras Nas ajulikanaye pia kwa jina halisi la Nasibu Mwanukuzi anachanganya mitindo ya reggae na muziki wa dansi. Kama upo Oslo usikose kujionea mwenyewe kwa macho yako. Usingoje kuambiwa!


Tarehe: Ijumaa 28 January

Mahali: Belleville, Cosmopolite (Vogstgate 64)
Shoo: Kuanzia 22.00 hrs


Shoo: Kuanzia 22.00 hrs

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA