TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, June 22, 2010

EAC imeridhia muundo wa sheria za mtandao kuinua uchumi na uwekezaji

5:11 PM

Mkutano wa siku tatu wa kitengo cha utendaji cha jumuiya ya Afrika ya Mashariki kuhusu sheria za matumizi ya mtandao umemalizika leo mjini Kigali Rwanda.

Kwenye mkutano huo wajumbe walijikita katika kutekeleza muundo wa sheria za mtandao zilizopitishwa hivi karibuni na baraza la jumuiya ya Afrika ya Mashariki, lililohusisha mawaziri wa usafiri, mawasiliano na hali ya hewa. Muundo huo ulitayarishwa kwa msaada wa UNCTAD ambapo maafisa wa serikali wa jumuiya ya afrika Mashariki watayapa uzito masuala ya kisheria kama haki ya umilikaji wa nyumba, ushindani wa kibiashra, masuala ya kodi za mtandao na usalama.

Nchi wanachama wanafikiria kurudhia sheria hizo za mtandao ambazo ni muhimu kwa kutekeleza huduma za kiteknolojia za serikali na kuongeza biashara na uwekezaji wa kikanda.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA