TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, March 30, 2010

wanafunzi wajifunza mambo ya tanzania

4:30 PM

Wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali ambao waliichagua Tanzania kama nchi wanayoiwakilisha katika Baraza hilo. Na ili waifanye kazi hiyo vema, wanafunzi hao waliutembelea Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa ili kujifunza na kupata uelewa zaidi kuhusu historia ya Tanzania, matatizo, mafanikio , changamoto, na namna gani Tanzania inavyoutumia Umoja Mataifa kusukuma ajenda zake mbalimbali. Aliyevaa suti nyekudu ni Afisa Ubalozi Bi Joyce Kafanabo ambaye alitoa maelezo na kujibu maswali mbalimbali ya wanafunzi hao, kwa niaba ya Balozi.
Kila mwaka wanafunzi wa shule za sekondari kutoka mataifa mbalimbali, hukusanyika na kuunda Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, (Model United Nations) Baraza hili ambalo ni la kuigiza lakini linalozingatia na kufuata sheria na taratibu zote za uendeleshaji wa Baraza Kuu halisia, huwapa fursa wanafunzi hao kuvaa viatu vya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa.

Kupitia Baraza lao, wanafunzi hao huendesha mijadala katika Nyanja mbalimbali kama vile masuala ya uchumi, mabadiliko ya tabia nchi, malengo ya maendeleo ya millennia, nafasi ya nchi zinazoendelea, ulinzi na usalama n.k. wanafunzi hawa hujenga hoja na kuzitetea hoja hizo katika mijadala hiyo kuligana ‘interest’ ya nchi wanayoiwakilisha.

Kupitia mijadala hiyo, wanafunzi hao hujaribu kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinazoikabili dunia hivi sasa, kwa kuandaa rasimu za maazimio na kuzijadili rasimu hizo na hatimaye kuzipitisha iwe kwa kuzipigia kura au kwa kuzipitisha kwa kauli moja.

Na ili kufanikisha mijadala ya baraza hilo, wanafunzi hao hufanya utafiti wa nchi zile wanazotaka kuziwakilisha katika baraza hilo pamoja na mada na ajenda mbalimbali.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA