Katika mazungumzo na rais Harmid Karzai mjini Kabul, rais Obama, amesema nchi hiyo imepiga hatua kubwa hususan upande wa kijeshi lakini amekiri kuna masuala mengi ambayo yanahitaji kutekelezwa. Rais Obama amesema raia wa nchi hiyo wanapaswa kujitolea zaidi kupambana na ufisadi na kukuza misingi ya utawala wa kisheria.
Baada ya mkutano na rais Karzai, rais Obama aliwahutubia wajeshi wa Marekani katika kambi ya Bagram. Obama aligusia haja ya kukabiliana vikali na wapiganaji wa Taleban pamoja na wale wa Al Qaeda .
Mwandishi wa BBC mjini Kabul amesema tangazo kuwa marekani haitaondoa majeshi yake nchini humo wakati wowote ujao, ni tangazo ambalo lilikuwa likisubiriwa na raia wengi wa nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment