TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Monday, February 15, 2010

Mawaziri waliosimamishwa Kazi Kenya wasalia afisini

7:36 PM

Mawaziri wawili wa serikali ya Kenya wameendelea na shughuli zao kama kawaida, baada ya utenda kazi wao kuzua mgogoro kati ya rais na waziri mkuu hali inayotishia kuleta mgawanyiko katika serikali ya muungano.

Mawaziri William Ruto wa Kilimo na Pro Sam Ongeri wa elimu walisimamishwa kazi na waziri mkuu Raila Odinga kufuatia kashfa ya mamilioni ya dola katika wizara zao.

Hata hivyo rais Mwai Kibaki alibatilisha hatua ya Odinga akisema waziri mkuu hana mamlaka ya kuwasimamisha kazi mawaziri. Ruto na Ongeri wameendelea kujitetea dhidi ya lawama yeyote.

Wakati huo huo Marekani imeonya kuzuka kwa machafuko ya kisiasa nchini Kenya kufuatia mgogoro wa sasa.

Kenya ilikumbwa na machafuko mengine miaka miwili iliyopita kufuatia uchaguzi mkuu uliokumbwa na utata ambapo zaidi ya watu elfu moja walikufa na maelfu kuachwa bila makao.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA