Sherehe za kuukaribisha Mwaka Mpya 2010 Tokyo
Jumuiya ya Watanzania Wanaoishi Nchini Japani (Tanzanite Society) inapenda kuchukuwa fursa hii kuwatangazia Watanzania wote wa Kanto na maeneo ya jirani na wale watakaokuwa wanatembelea Kanto wakati huu wa kipindi hiki cha Mwaka mpya kuwa kutakuwa na sherehe kabambe ya kuukaribisha mwaka mpya (2010). Sherehe hizi zitafanyika huko Mkoani Kanagawa. Maelezo kamili ya shughuli hiyo ni kama ifuatavyo:-Siku: 3/1/2010 (Jumapili)Muda: Kuanzia saa tatu usiku mpaka majogooKiingilio: Yeni 1500 (utapata kinywaji kimoja)Ukumbi: Amore Club uliopo ghorofa ya pili ya jengo la Grande Hon Asugi, Hon Asugi, Nakacho-2-13-13, ilipofanyikia sherehe ya Uwataja 2008 (Karibu na ukumbi wa mama Mperu). Dakika 5 toka kituo cha train cha Hon Asugi (Odakyu line)Muziki: DJ mkongwe, DJ Zee atakupatia miziki ya aina mbalimbali kuanzia zile za kizazi cha zamani (enzi za mababu zetu) mpaka za kizazi cha kipya, hip hop, taarab, nk.Kwa ufafanuzi na maelekezo ya ziada tafadhali wasiliana na wanakamati wa kamati ya uhamasishaji na Starehe:Bw Pembe: 080-3458-8786Bi Angela: 080-3397-0339Bi Upendo: 080-1326-9700Bi Mariam: 090-4422-8555Bw Ntale: 080-4149-1257Tunawaomba watanzania pamoja na marafiki zao wa mataifa mengine kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha shughuli hii. Ukipata taarifa hii mtaarifu na mwenzio.AhsanteKamati ya Uhamasishaji na StareheJumuiya ya Watanzania Wanaoishi Nchini Japani
Home
»
»Unlabelled
» Sherehe za kuukaribisha mwaka mpya 2010 Tokyo
Sherehe za kuukaribisha mwaka mpya 2010 Tokyo
4:01 PM
Mshirikishe Mwezako Kupitia:
0 comments:
Post a Comment