TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, November 3, 2009

Mkurugenzi wa kupambana na rushwa agoma kujiuzulu

3:58 PM

Ramadhan Semtawa

MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah amekoleza moto wa mjadala wa Bunge kuhusu utendaji wa taasisi yake baada ya kujitokeza hadharani na kueleza kuwa hana mpango wa kujiuzulu.

Na kama haitoshi, Dk Hoseah amesema wabunge hawamtaki, wapige kura za kutokuwa na imani naye, ikiwa ni siku mbili kabla ya Bunge kujadili taarifa ya serikali ya utekelezaji wa maazimio ya chombo hicho kesho, kama alivyoahidi Spika Samuel Sitta.

Katika maazimio hayo kuhusu kashfa ya utoaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development LLC, Dk Hoseah anatakiwa kuwajibishwa na mamlaka ya juu kutokana na taasisi yake kushindwa kubaini rushwa katika utoaji wa zabuni hiyo.

Hoseah, aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari ambao kila mmoja alipewa kipeperushi kinachotoa ufafanuzi wa athari za malipo yasiyostahili kwa watumishi wa umma na adhabu zake, alionekana ni mwenye jazba, msimamo na kujiamini, licha ya joto la uchunguzi huo na shinikizo la wabunge kutaka awajibishwe, kuwa juu.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA