Maafisa waliopo katika mazungumzo ya kugawana madaraka huko Madagascar wamesema wapinzani wa kisiasa kisiwani humo wamefikia muafaka wa nafasi za uwaziri katika serikali mpya ya muungano. Taarifa hizo zimetolewa baada ya kuwepo na majadiliano kwa wiki kadhaa yaliyokusudia kumaliza mgogoro wa kisiasa ulioanza mapema mwaka huu.
Katika makubaliano hayo, Andry Rajoelina anaendelea kuwa rais wa kisiwa hicho.
Bw Rajoelina alimwondosha aliyekuwa rais wa kisiwa hicho Marc Ravalomanana mwezi Machi akiungwa mkono na jeshi la kisiwa hicho.
Kuondoshwa kwa Bw Ravalomanan kulitokea miezi kadhaa baada ya kuwepo na maandamano ya kuipinga serikali yake.
0 comments:
Post a Comment