
Mahakama ya Sudan imekubali kutoa hukumu ya kifo dhidi ya wapiganaji wanne wa kiislam nchini humo.
Wapigananji hao wamepatikana na hatia ya kumpiga risasi na kumwuua mjumbe mmoja kutoka Marekani mwezi Januari 2008.
John Granville, 33, na dereva wake ambaye ni raia wa Sudan Abdelrahman Abbas Rahama waliuawa walipokuwa wakirudi katika sherehe za mwaka mpya mjini Khartoum.
Hapo awali mama yake Granville aliomba hukumu hiyo ya kifo ipitishwe.
Katika sheria za kiislamu za Sudan, familia iliyopoteza ndugu yake kwa kuuawa ina uwezo wa kumuombea msamaha mshatkiwa asihukumiwe kifo au kuomba fidia.
0 comments:
Post a Comment